KEMBAKI NITATATUA CHANGAMOTO.



KEMBAKI NITATATUA CHANGAMOTO.

MBOMBEA Ubunge jimbo la Tarime Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Michael Kembaki amesema Wananchi wakimchagua kuwa Mbunge atatatua changamoto zinazowakabili.

Kembaki aliyasema hayo hivi karibuni wakati akihutubia wananchi waliohudhuria mkutano wa uzinduzi wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Buhemba shule ya msingi Mazoezi wilayani hapa.  

;; Endapo mkinichagua kuwa Mbunge wenu nitahakikisha ninatatua  changamoto na kero za jimbo hili zinazowakabili kama vile maji,wajasilia mali kuwezeshwa kupata mikopo yenye riba ya garama nafuu ili kuinua uchumi,pia Elimu na afya  zitaborshwa;;alisema Kembaki.

Mgombea huyo alisema kuwa jimbo hilo  ni jipya na atahakikisha Amani inakuwepo kwa lengo la wawekezaji kuja kuwekeza na wananchi wake hususani vijana kujipatia Ajira.  

 Aidha kembakai aliongeza kuwa katika sekta ya elimu atzidi kuboresha kwa lengo la kuwajengea wanafunzi kuazia shule za msingi kupenda shule.

Naye Mgombea Ubunge Jimbo la Tarime Vijijini  Christopher Kangoye alisema kuwa Magufuri anauzalendo na nchi yake ni mchapakazi anachukia rushwa nakwamba wakimchagua hawatajuta kwani wanaotaka mabadiliko hawajawahi kufanya mabadiliko yoyote.

“Uzalendo alionao magufuli utasaidia kiasai kikubwa kuleta madadiliko endapo wananchi watakuwa tayari kumpa ridhaa ya kuongoza” alisema Kangoye.

Kwa upande wake Katibu Uchumi wa Chama cha mapinduzi wilaya Tarime John Gimunta alisema kuwa wananchi waamini chama cha mapinduzi kwa kuwa kina Ilani na Sera za maendeleo.

‘’Wananchi chagueni CCM Chama cha Amani chenye maendeleo kwa Wananchi wake ambacho kina sera dhabiti kuliko vyama vingine vya siasa vijana jua mabadiliko mtayapata ndani ya CCM;;alema Gimunta. 

Aidha Gimunta aliongeza kuwa wananchi wakimpa Michael Kembaki ambaye ni mgombea wa jimbo la Mjini watakuwa wamechagua chaguo sahii siovinginevyo.

Powered by Blogger.