Masurura FC bingwa kombe la Sabega cup

Kulia ni mdhamini wa ligi hiyo Sabega Cup 2015 Fredy Sabega akikabidhi kapten wa Timu ya Masurura Fc baada ya kuilaza Kemange Fc kichapo cha bao1-0 kupitia mkwaju wa penaliti na kuibuka washindi na kujinyakulia kitita cha shilingi laki Nne.


  Masurura FC  bingwa kombe la Sabega cup
                             Tarime
LIGI ya iliyopewa jina la Sabega imemalizika huku timu ya Masurura ikiibuka bingwa msimu wa 2015 kwa usindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Kemange FC kwenye mchezo wa fainali uliyochezewa kwenye uwanja wa Kemange shule ya msingi, halmashauri ya mji wa Tarime mkoani Mara.

 Bao pekee la timu ya Masurura lilifungwa na Jaliwa Alkard dakika ya 72 kwa  mkwaju wa penaliti baada ya mchezaji huyo kutendewa madhambi eneo la hatari la lango la timu ya Kemange  ambapo mwamuzi mwenye beji ya FIFA Sophia Mtongori aliamua kutengwa kwa penaliti hiyo.

 Mshindi  huyo wa kwanza (Masurura) waliibuka na kitita cha  sh, 400,000 na kikombe cha thamani y ash, 300,000, mshindi wa pili (Kemange) aliibuka na sh, 300,000 na kikombe cha thamani ya sh, 200,000huku mshindi wa tatu Nyamonkanga aliibuka na sh, 150,000 na kikombe chenye thamani y ash, 100,000. 

Nahodha wa timu ya Masurura Ignas Ponsiano alisema kuwa ilikuwa ni halali yao kuibuka mabingwa wa ligi hiyo kwa kuwa tangu michuano hiyo inanze juni 23 na kumalizika julai 12 hawakuwahi kupoteza hata mchezo mmoja kutokana na hali hiyo ushindi huo ulikuwa ni wao.

Kwa upande wake kocha  wa Kemange FC Samwel Mwita ambao walikuwa wenyeji wa uwanja huo ameiambia blog hii kuwa  amepokea ushindi wa namba mbili kama changamoto kwake kama kocha na kuwa waonyeshwa kuwa bado wanahitajika kufanya juhudi kwa ili kuwa mabingwa msimu ujao.

Naye mdhamini wa ligi hiyo Fredy Sabega alisema  mwaka wa nne ameona wachezaji wazuri tofauti na miaka mingine ambayo ilimfanya akataka kukata tamaa hivyo  viwango vyao vya kisoka  kufikia katika kiwango ambacho wanaweza kuuzika katika timu kubwa za kitaifa.

“Lengo langu ni kuona vijana wanaibua vipaji vya soka katika kata ya Nyandoto nimeona ndoto nyangu  inaenda kutimia kwani huu ni mwaka wangu wa nne tangu nilipopata wazo la kuwakusanya vijana ili kuleta umoja na kuwafanya wasiingie kwenye masuala ya uhalifu viwango vyao vya soka vimepanda… wanaohitaji vijana kwa ajili ya timu zao nawaomba wafike katika kata ya Nyandoto” alisema Sabega.

Sebaga aliongeza kuwa ratiba rasimi tayari ipo katika chama cha mpira wilaya hivyo kila mwaka kutakuwepo na mashindano kwa lengo la kukusanya vijana kwa pamoja kwa lengo la kuepukana na vishawishi kama vile Ngono zembe madawa ya kulevya hivyo muda mwingi watautumia katika michezo.

                                                Mwisho.
Powered by Blogger.