MAKADA 109 WARUDISHA FOMU YA KUGOMBEA NAFASI YA UDIWANI TARIME/RORYA.



                                 Tarime.

MAKADA 109 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wiki hii wamerudisha Fomu ya kugombea nafasi ya Udiwani Wilayani Tarime na Rorya mkoani Mara.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katibu baraza la Wazee Chadema wilaya Tarime Samsoni Sanda amesema kuwa kati ya 105 waliorudisha fomu kwa jimbo la Tarime 46 ni viti maalumu.

Aidha Sanda ameongeza kuwa  mchakato huo ulianza Juni 19 hadi kukamilika Julai 10 mwaka huu ambao siku hiyo  ndiyo ilikuwa mwisho wa kurudisha fomu za kuwania kuomba nafasi ya Udiwani.

Kwa upande wa jimbo la Rorya makada 4 akiwamo Diwani Thomasi Partrick Lisa   na wenzake wawili wamerudisha fomu ya kugombea nafasi ya udiwani kukamilisha idadi ya watia nia Tarime na nRorya kufikia 109.

Thomasi Patrick amesema kuwa akifanikiwa kuteuliwa na kupitishwa na chama chake atahakikisha barabara ambazo zinaleta kero ndani ya kata yake ya Kitembe pamoja na Wilayanzima ya Rorya barabara zinapitika kwani katika awamu nyingine diwani huyo amechukua fomu ya kuwania ubunge wa jimbo la  Rorya   sanjari na kuongeza ufanisi wa ufaulu kwa wanafunzi.

Wengine waliorudisha fomu ya kugombea nafasi ya udiwani kata ya Kitembe kupitia CHADEMA ni pamoja na Kerina Oyuma na Mery Thomasi Makodede Makodede wakata ya Bukwe Wiliamu Otuki kata ya Roche alisema Gradus Festo Ndira mwenyekiti CHADEMA Kata ya kitembe.

Mmoja wa watia nia Mtoto wa marehemu Chacha Wangwe ambaye aliwahiu kuwa mbunge wa jimbo la Tarime kupitia CHADEMA,Zakayo Chacha Wangwe aliwambia waandishi wa habari kuwa kama chama chake kama kitamteuwa na kuwa mgombea udiwa ani kata ya Turwa Wilayani Tarime atahakikisha anashirikiana na wananchi wake kuwaletea maendeleo.

Aidha Zakayo ameongeza kuwa endapo atafanikiwa kuingia halmashauri atatumia nafasi yake kushawishi madiwani wenzake kubuni vyanzo  vipya  vya  mapato ili kuingizia halmashauri fedha ya kuendeshea miradi ya maendeleo kwa wananchi wa Tarime na Tanzania kwa ujumla.

Powered by Blogger.