Ubalozi wa china wakabidhi maabara katika shule ya Msingi aliyosoma Baba Taifa.

Picha ya Balozi wa China Dr Lu Youqing kulia wa kwanza akikata utepe katika uzinduzi wa Maabara ya kisasa iliyojengwa na ubalozi wa china katika shule ya Msingi Mwisenge ambapo alisoma Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Mara Aseri Msangi akifuatiwa Meya wa Manispaaya Musoma Alex Kisurura



Ubalozi wa china wakabidhi maabara katika shule ya Msingi aliyosoma Baba Taifa.

Ikiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Murisho kikweteanatilia mkazo ujenzi wa maabara tatu kwa kila shule za Sekondari hapa Nchi  kwa lengo la kuongeza ufauru mkubwa katika masomo hayo,Ubalozi wa China  kupitia balozi wake Dr Lu Youqing wamekabadhi Maabara moja katika shule ya Msingi Mwisenge iliyopo  manispaa ya Musoma  ambayo ni moja ya Shule aliyesoma Baba wa Taifa Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere kwa lengo la kuchochea masomo ya sayansi kwa watoto wa shule za msingi kusoma masomo hayo kwa vitendoikiwa ni pamoaj na kuenzi Baba wa Taifa.

Akikabidhi maabara hiyo Balozi wa China amesema kuwa maabara hiyo imejengwa kwa lengo la kumuenzi wa wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere  katika uhai wake kwani alichangia kwa kiasai kikubwa kuleta mahusiano mema baina ya Nchi ya Tanzania na  ubalozoi wa China huku akisema kuwa Mwl Nyerere alikuwa Mwanasiasa wa kueshiiwa na Mwanzilishi wa ukombozi wa Bara la Afrika.

“Mwalimu Nyerere alikuwarafikimzuri wa China pamoja na Mwenyekiti Mao Zedong, Waziri Mkuu Zhou Enlai na Viongozi wengine wa China wao waliweza kupanda mbegu ya Urafiki baina ya Nchi ya Tanzania na Ubalozi wa China” alisema Dr Lu Youqing.

Aliongeza kuwa Ubalozi wa china umeanza kutoa tuzo kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo ikiwa ni pamoja na kujenga masomo moja.

“Rais kikwete anatilia mkazo sana katika masomo ya sayansi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa maabara ni maamuzi sahihi ya kimkakati katika kukuza Viwanda na kukuza uchumi wa Taifa la Tanzani” alisema Balozi.


Akisoma Risala mbele ya Mgeni rasimi Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Mwisenge Elias Makoro aliweza kutoa historia fupi ya shule hiyo huku akisema kuwa shule hiyo wameweweza kusoma viongozi wakubwa wakitaifa hivyo aina budi kupewa kipaumbele katika kuiboresha na kuwa mfano bora katika shule zote zilizomokatika Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.


Mkuu wa Mkoa wa Mara Aseri Msangi alisdema kuwa uwepo wa maabara katika Shule ya Msingi Mwisenge itakuwa chachu kubwa ya kusoma masomo ya sayansi.

“Tunatia shukrani zetu katika ubalozi wa china uwepo wa Maabara hii itakuwa chachu kubwa ya watoto wetu kusomA Masomo ya Sayansi” alisema Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Makongoro Nyerere ni Mbunge wa Afrika Mashariki alisema kuwa mahusiano mazuri na urafiki ulikuwepo na Hayati Baba wa Taifa na Viongozi wa Balozi wa China umesababisha kujengwa kwa maabara katika shule ya Msingi ambayo alisoma Julius Kambarage Nyerere.

“Watoto wetu hawatasahau msaada huu ambao mumeweza kutoa nyie  ubalozi wa china” alisema.


Kwa Upande wake meya wa manispaa ya Musoma Alex Kisurura alitoa shukrani zake kwa ubalozi wa China  kwa niaba wakazi wote wa Musoma kwa Msaada huo wa ujenzi wa Maabara katika shule ya Msingi kwani ni Shule ya kwanz Mkoani Mara kuwa na Maabara katika shule za Msingi.

Sanjari na hayo balozi wa china alisema kuwa kuwa mbali na kukabidhi  Maabara hiyo ataweza kuleta na vifaa vyake ili wanafunzi waweze kusoma mara moja kwa vitendo n kuongeza ufauru.
......M wisho...
Powered by Blogger.