Wazee wa mila wahapa mbele ya Dc Tarime


                                                   Tarime
    
Wazee wa mila kutoka koo zote za kabila la  Wakurya   Wilayani Tarime  Mkoani Mara  wamekubaliana   kuacha  kukeketa  watoto wa kike mbele  ya Mkuu wa  Wilya  Tarime(DC)  John  Henjewele nakusema kuwa Wasichana sasa  kupakwa unga ili  kuendelea  kudhumisha  mila zao

Wazee  hao walisema kuwa  kuanzia sasa  watoto  wa kike ambao wamefikisha umri wa miaka 17  watakuwa  wakipakwa unga usoni  kama ishara  ya  kudumisha  mila hiyo   kila  inapofika  wakati  wake
“  Kuanzia  sasa mheshimiwa  DC  hili jambo la ukeketaji  tumelimaliza.   Ila sherehe  zote zitakuwa zikifanyika lakini  kukeketa  hapana”,  wazee  hao walisema  katika  kikao kilichofanyika katika ofisi ya DC  Henjewele  hivi karibuni.

Kikao  hicho kilikuwa  chini ya uenyekiti wa  DC  Henjewele na   kiliwezeshwa  na  Shirika la Jukwa la Utu wa Mtoto(CDF)  kwa  ufadhili  wa  Shirika la Umoja wa  Mataifa la Idadi ya Watu(UNFPA) na Tasisi ya  Graca Machel Trust.

 Kikao hicho  kilihudhuliwa pia  na Mkurungenzi Mtendaji wa  Halmashuri ya  Wilaya  ya  Tarime Athuman Akalama na   maafisa  wa polisi  kutoka  ofisi ya  kamanda   wa mkoa  wa kipolisi wa  Tarime Rorya.

Hata hivyoWazee  hao  walisema  kila mwaka wamekuwa  wakipiga hatua  katika  kuitikia wito wa serikali na kuacha kukeketa  watoto wa kike.

“ Miaka ya hivi karibuni  tulikuwa tunaketeka ki-CCM bila kuwaumiza watoto  lakini  tumeanza kuwapaka unga ili tu kudumisha mila na  sasa  itakuwa  ni  kupaka unga tu na hakuna kukeketa”,  walisema.
“ Leo  tumetamka kuwa  ukeketaji   Tarime  hakuna  na hata  aliyepanga  kutukamata  hatatupata tena”, alisema  mmoja wa wazee  hao.
Wazee  hao  walikubaliana  kuanza  kusadia kutoa  elimu  dhidi ya ukeketaji   katika maeneo yao ili kuweza kuwashawishi baadhu ya wazee ambao wanaendekeza masua;la haya ya kimila.
DC  Henjewele  aliwashukuru  wazee  hao kwa kukubali  kuachana  na  ukeketaji  lakini  akaonya kuwa zoezi hilo la kupaka unga  lisije likatumiwa  vibaya .

“  Tuiialike  na sisi  hata kwenye  hizo  za  sherehe za kupaka unga ,  zoezi hilo lisiitwe ukeketaji, litafutiwe jina lingine  na kuruhusu  watu wapige hata  picha  ili kuonesha hakuna ukeketaji tena  Tarime na tusije kupata ushadi wa mtoto  kukeketwa”,  alisema  DC  Henjewele.
“   Serikali  bado inahitaji msaada wenu wazee  wangu ili  tuondakane na aibu hii. Leo mmeifurahisha serikali”,  Mkuu huyo  wa wilaya aliawambia  wazee hao .

DC henjewele   aliunda kamati  maalumu ambayo  itasimamia   na kufutilia utekelezaji wa makubaliano katika kikao hicho ikiwa ni pamja na kuangalia  shughuli mbadala  zitakazokuwa zinafanywa na wazee  hao  baada ya kukubali  kuachana  na ukeketaji. Kamati hiyo tayari imeeanza kazi yake.

                                                                     Mwisho


Powered by Blogger.