Migogoro ya kifamilia chanzo kikubwa kwa mabinti mkufanya bihashara ya kingono

Elieth Samsoni kutoka dawati la jinsia manispaa ya Musoma Mkoani Mara akiwasilisha mada juu ya watoto ambao wamejiingiza katika bihashara ya ngono ni katika kikao cha wadau kilchofanyika leo kwenye ukumbi wa shirika la Center For Widows and Children Assistance lililopo Mjini Musom


Imebanishwa kuwa migogoro ni chanzo kikubwa cha usababishi wa watoto wadogo ususani mabinti kujiingiza katika suala zima la bihashara ya kingono katika wilaya ya Butiama, Musoma Mjini na Musomavijijini Mkoani Mara, suala ambalo upelekea mabinti hao kupata mimba za utotoni pamoja na maambukizi ya virusi vya ukimwa na Magonjwa ya zinaa.
Hayo yamebainishwa katika kikao cha wadau kwenye ukumbi wa Ofisi za Shirika la Center For Widows and Children Assistance zilizopo Manispaa ya Musoma Mkoani  Mara kwa kuusisha wadau kutoka taasisi mbalimbali kama vile, Maofisa ustawi wa jamii, Wasaidizi wa kisheria, watendaji wa kati , Weneviti wa vijijina Vitongoji, Mashirika ya utetezi wa haki zabinadamu,Wandishi wa habri na Maofisa kazi kutoka katika wilaya za Butihama, Musoma mjini na Musoma Vijijini.
Katika kuchangia mada zilizowekwa mezani wadau hao walisema kuwa Migogoro inapoingila katika family wazazi upelekea kutelekeza familia na kufanya watoto kujitunza wenyewe na kupelekea kkujiingiza katika vishawishi vya kingono.

“Baba au Mama wanapokimbia familia upelekea watoto kujitunza wenyewe suala ambalo upelekea kuijiingiza katika masuala ya kingono kwa ajili ya kupata kipato cha kuendesha familia hizo” walisema wadau hao.
Ofisa Mwandamizi wa shirika la Center For Widows and Childres assistance Ostack Mligo ambao pia ni wawezeshaji wa mdharo huo alisema kuwa lengo kubwa la kukutanisha wadau hao ni kuangali namna ya kunusuru watoto ambao tayari wamejiingiza katika bihashara za kingono Mkoani Mara ili kuweza kuwasaidia
“Lengo kubwa ni kuona kipi kifanyike, chanzo kikubwa ni nini kwani watoto wetu wanazidi kuangamia kutokana na bihashara hizi za kingono” alisema Mligo.
Elieth  Samsoni  kutoka katika dawati la jinsia katika manispaa ya Musoma  alizitaja changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi ili kutokomeza vitendo vya ukatili vinavyozidi kutendeka hapa nchini alisema kuwa baadhi nya Watendaji wa kata, wenyeviti wa Vijiji, na Vitongoji wamekuwa wakihamua kesi na kupelekea kupotea kwa ushaidi.
“Sisi dawati la jinsia na wtoto tukifuatilia kesi za watuhumiwa vijijini wakatimwa kufika eneo la tukio tunakuta tayari watendaji wa kata vijijina vitongoji wamekaa mezani na kumaliza kazi” alisema Elieth.
Kwa upande wake  diwani wa kata ya Buhare Lukas Masige alilahani kitendo cha wenyeviti wa vijiji na watendaji wa kata ambao wamekuwa mihungu watu na  kuzidi kuwanyanyaja wananchi wao pale wanapoitaji huduma.
Licha ya hayo wadau walisema kuna aja kubwa ya kuhusisha walimu, Wazazi wote wawili Baba na Mama katika washa zinazoandaliwa kwani uka na watoto kwa mda mwingi ili kuweza kutokomeza vitendo vya ukatili vinavyotendeka.
“Mashuleni walimu ndio walezi wakubwa haebu jaribu kuwashirikisha katika mijadala kama hii ili kuweza kutimiza ndoto zenu nyie kama asasizisizokuwa za kiserikali ambazo zimeamua kumkomboa mtoto wa Tanzania” walisema.
                                                     ……MWISHO…
Powered by Blogger.