Mwenyekiti, VEO wanusurika kipigo wajumbe serikali ya kijiji:



Mwenyekiti, VEO wanusurika kipigo wajumbe serikali ya kijiji

Kikao cha serikali ya kijiji cha Sirari kilishindwa kuendelea baada ya wajumbe kudai kukerwa na kauli ya mwenyekiti wa kijiji hicho  Nyangoko Romani kwa kuwambia wajum be hao kuwa ajenda ya kupitisha bajeti haitakuwepo maana wevyeviti wa vitongoji hawakupeleka bajeti yao.

Hali hiyo ilizua taharuki ndani ya kikao na kuwafanya wajumbe kuanza kurushiana matusi na kutishiana kiasi cha kupigana makonde hali iliyokifanya kikao kukatishwa muda mfupi baada ya kuanza. Sauti zilisikika zikisema  “tunataka posho yetu huwezi kutuita hapa kupanga bajeti na posho yetu tusipate”

Wakiongea kwa jabiza juu ya kuomba fedha yao ya malipo ya mwaka mzima  kwa wenyeviti vitongoji ambayo ni  sh, 60,000, mmoja wao aliyejitambulisha kwa jila la Robert Mashon alisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiambiwa kupewa posho, na sasa kijiji kimepata fedha kutoka Halmashauri ya Wilaya  ya sh, 2.5 milioni.

“Fedha imekaa banki inaendelea kupungua ikikatwa bila kutumika, tupewe posho yetu  ya mwaka sh, 60,000 na nyingine tuingize kwenye matumizi ya kijiji kuliko kukaa humo inaendelea kukatwa” alisema Robert.

Na kuongeza kuwa, mkutano wa serikali ya kijiji uliitwa ili kupanga bajeti, lakini baada ya kusaini mahudhurio mwenyekiti aliswambia kuwa ajenda ya bajeti isubiri kwanza hadi hapo wenyeviti hao watakapoonyesha katika vitongoji vyao wanataka kufanya nini ili wapewe fedha hizo.

Hata hivyo Nyangoko Romani alisema kuwa wenyeviti wa vitongoji hawakuwa na bajeti ya vitongoji vyao hivyo ikaonekana kuwa watakapo pewa fedha hizo watazitumia kinyume  na kuwaomba waandae bajeti yao itakayoonyesha kiasi cha fedha wanachokitaka na kinaenda kufanya nini ndipo wapitishe bajeti ya kijiji hicho.

“Wanapoitwa kwenye shughuli za maendeleo hawaji na pengine huja mmoja leo wamesikia mkutano wa bajeti wote wamefika, tena kwa kupigiana simu, na cha kushangaza hawakuwa na bajeti ya vijiji vyao” alisena Romani muda mfupi baada ya kikao hicho kushindwa kuendelea.

Mtendaji wa kijiji hicho Mirumbe Mirume alisema kuwa kushindwa kukamilika kwa mkutano wa serikali ya kijiji kunamfanya yeye ashindwe kutekeleza majukumu yake ipasavyoa kwani anaitegemea serikali hiyo kupitisha maamuzi ili yeye ayafanyie kazi.

“Nashindwa kutekeleza majukumu yangu kutokana na wajumbe hawa kutokuwa makini kufanya maamuzi, na wakati mwinmgine naweza nikaonekana mimi ni mzembe.

Hata hivyo mtendaji wa kata hiyoa ya Sirari Paulo Maisori alisema kuwa Sirari ni moja ya kata ambazo watu ni wabishi na wakali wanapotakiwa kufanya shughuli za maendeleo.

“Nimepita katika kata na vikao vya serikali za vijiji nyingi lakini sijawahi kuona kijiji kama hiki, watu ni wabishi ukiongea wanaamka wanataka kukupiga badala ya kuangalia maendeleo  ya kijiji chao, kushindwa kufanyika kwa kikao hicho kwa kumshabulia mwenyekiti na mtendaji ni kwa sababu wamekuwa wakaidi wao wanadai  posho yao y ash, 5000 kila mwezi kwa mwaka mmoja sh, 60,000 bila kuonesha juhudi za kushiriki katika maendeleo” alisema Maisori.

                                  ……..MWISHO….
Powered by Blogger.