TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA YAJIDHATITI KUKUZA ELIMU NCHINI



Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Bureta akizungumza na wadau wa Elimu ya Watu Wazima wakati wa warsha iliyolenga kuibua mbinu na mikakati ya kusaidia kufuta ujinga wa kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa vijana na watoto. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt. Fidelice Mafumiko. Warsha hiyo ilifanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt. Fidelice Mafumiko akizungumza na wadau wa sekta ya elimu wakati wa warsha ya utoaji maoni kuhusu mpango wa utoaji elimu kwa makundi maalum ya vijana na watoto walio chini ya umri wa miaka 17. Kushoto ni Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Buretta. Warsha hiyo ilifanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi wa Taaluma, Utafiti na Ushauri kutoka Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) Dkt. Kassimu Nihuka akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Fidelice Mafumiko (wa pili kulia) kutoa taarifa kuhusu malengo ya semina kwa wadau wa elimu iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es salaam.


Kaimu  Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Buretta (katikati) akisisitiza jambo kwa washiriki wa semina hiyo. Warsha hiyo ilifanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.

.Baadhi ya washiriki wa warsha ya wadau wa elimu iliyoratibiwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Tanzania (TEWW) wakifuatilia hotuba ya Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Buretta (hayupo pichani). Warsha hiyo ilifanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
Kaimu  Kamishna wa Elimu toka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Buretta (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa semina ya wadau wa elimu  iliyoratibiwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Tanzania iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
 ( Picha na Frank Mvungi )
Frank Mvungi
Taasisi ya Elimu ya Watu wazima Tanzania (TEWW) imedhamiria kuondoa changamoto ya Watanzania wasiojua kusoma na kuandika hapa nchini hasa vijana walio chini ya umri wa miaka 17.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicolas Buretta wakati akifungua warsha ya siku moja ya wadau wa Elimu iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
“Tunalenga kuwafikia watoto ambao hawajapata kabisa fursa ya kupata elimu kwa sababu ya umaskini au mazingira na pia tunalenga kuwafikia watoto wote walio na umri chini ya miaka 17” Alisisitiza Buretta.
Akifafanua Buretta amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata haki ya kupata elimu bora ili kuzalisha wataalamu wenye ujuzi, uwezo na weledi watakaosaidia kujenga uchumi wa viwanda.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt. Fidelice Mafumiko alisema kuwa mpango huo unatoa kipaumbele kwa wale waliokosa elimu kupitia  mfumo rasmi ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata elimu.
“Dhamira ya Taasisi ya Elimu ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na mfumo nyumbufu utakaowezesha Watanzania wote wanapata elimu iwe katika mfumo rasmi au usio rasmi” Alisisitiza Mafumiko.
Kwa upande wake Mtaalamu wa Elimu kutoka UNICEF Dkt. Ayoub Kafyulilo alisema kuwa maktaba za Kata zitasaidia kuongeza ari ya kujisomea miongoni mwa vijana na jamii kwa ujumla.
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) iko chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na ina jukumu la kuendeleza Elimu ya Watu Wazima (EWW) na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi nchini.A
Powered by Blogger.