MBEYA CITY UWANJANI TENA KESHO KUPAMBANA KUEPUKA SARE MFULULIZO
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL)
inatarajiwa kuendelea kuanzia kesho Alhamisi Aprili 13, 2017 kwa timu ya
Mbeya City itaikaribisha African Lyon ya Dar es Salaam kwenye Uwanja wa
Sokoine jijini Mbeya katika mchezo utakaoanza saa 10.00 jioni.
Kikosi cha Mbeya City kimekuwa
kikiandamazwa na sare mfululizo, jambo ambalo kesho kitakuwa kinapambana
kuhakikisha kinaepuka sare hizo na kuanza kukusanya pointi tatu.
Jumamosi ya Aprili 15, mwaka huu
kutakuwa na michezo minne ambako Stand United itakuwa mwenyeji wa Mtibwa
Sugar ya Morogoro kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga wakati
Toto Africans ya Mwanza itaialika Simba SC ya Dar es Salaam kwenye
Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mechi hizi, zitachezwa kuanzia saa
10.00 jioni.