HATA YANGA HAIJAFIKA ALGERIA, KIPA WA MC ALGER AFUNGWA JELA KWA UBABE
Wakati
Yanga inatarajia kutua nchini Algeria kesho, kips Faouzi Chaouchi, wa
MC Algiers amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela kwa
Chaouchi
ametikana na hatia ya kutumia nguvu ikiwa ni pamoja na kumdhalilisha
askari polisi wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Algeria, Februari 7, mwaka
huu.
Inaelezwa
katika mechi hiyo MC Alger dhidi ya NAH Dey, Chaouchi alianza kuzozana
na askari aliyekuwa akiwakagua wachezaji kwa ajili ya masuajua ya
usalama.
Pamoja na kifungo hicho cha miezi sita, Chaouchi ametakiwa kulipa faini ya dinar 50,000 zaidi ya Sh milioni 1 ya Tanzania.
Katika
mechi ya Kombe la Shirikisho iliyopigwa Dar es Salaam ambayo MC Alger
ililala kwa bao 1-0 dhidi ya Yanga, langoni akiwa yeye Chaouchi.