HATA YANGA HAIJAFIKA ALGERIA, KIPA WA MC ALGER AFUNGWA JELA KWA UBABE




Wakati Yanga inatarajia kutua nchini Algeria kesho, kips Faouzi Chaouchi, wa MC Algiers amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela kwa 

Chaouchi ametikana na hatia ya kutumia nguvu ikiwa ni pamoja na kumdhalilisha askari polisi wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Algeria, Februari 7, mwaka huu.
Inaelezwa katika mechi hiyo MC Alger dhidi ya NAH Dey, Chaouchi alianza kuzozana na askari aliyekuwa akiwakagua wachezaji kwa ajili ya masuajua ya usalama.
Pamoja na kifungo hicho cha miezi sita, Chaouchi ametakiwa kulipa faini ya dinar 50,000 zaidi ya Sh milioni 1 ya Tanzania.
Katika mechi ya Kombe la Shirikisho iliyopigwa Dar es Salaam ambayo MC Alger ililala kwa bao 1-0 dhidi ya Yanga, langoni akiwa yeye Chaouchi.
Powered by Blogger.