DC RORYA MADIWANI SHIRIKIANA KATIKA KUONGEZA PATO LA HALMASHAURI

Madiwani wilayani Rorya Mkoani Mara wakiwa katika kikao cha balaza la Madiwani robo ya pili ya Mwaka 2016-2017.

Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Charles Chacha anafuatiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Albert Machiwa katikati ni Mkuu wa wilaya ya Rorya Simon Chacha katika Balaza la Madiwani la Robo ya pili mwaka 2016-2017.


Wa kwanza kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Rorya Simon Chacha wa pili ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya Albert Machiwa wakiwa katika Balaza la Madiwani.



Kikao cha baraza la Madiwani Wilayani rorya Mkoani Mara kimekaa hii leo kwa lengo la kujadili taarifa za kata 26 zilizopo wilayani humo katika robo ya pili ya mwaka 2016-2017 Mkuu wa wilaya ya Rorya Simon Chacha amewataka madiwani hao  kuendelea kuimiza Waanchi wao kwa lengo la kulima chakula cha Muda mfupi ili kuondokana na upungufu wa chakula ambao unaweza kujitokeza Mbeleni.

“Waeshimiwa madiwani nadhami hali ya hewa munaiona hebu endelea kuimiza wananchi wajikite katika kutumia hizi mvua ambazo zinaendelea kunyesha ili kupata chakula” alisema Simon.

Mkuu wa wilaya pia ameipongeza Halmashauri hiyo katika suala zima la kuendelea kufanya vyema sekta ya elimu na kusema kuwa wilaya hiyo imetunikiwa hati ya utendaji bora na waziri wa Elimu,Sayansi, Teknologia na Ufundi  Profesa Joyce Ndalichako pamoja na fedha baada ya kufanya vizuri katika sekta ya Elimu.

Hivyo amewamba  madiwani kuendelea kushirikiana vyema kama walivyoshirikiana katika sekta ya elimu sasa washirikiane katika kukusanya mapato ya ndani ili Rorya iendelee kutekeleza miradi ya wanachi  ipasavyo.

Naye Mkurugenzi wa Wilaya hiyo Charles Chacha amesema kuwa wanaendelea na mikakati ili kuendelea kubuni vyanzo vya mapato kwa lengo la kuongeza kipato na kutekeleza miradi ya Wanchi katika Sekta zote ikiwemo Afya, Maji Elimu na Barabara.

Edward Ndege ni diwani wa kata ya Nyahongo amedai kuwa kwa sasa wilaya hiyo inakumbwa na upungufu wa chakula hivyo wameiomba Serikali kuona haja ya kuleta chakula cha bei nafuu ili wanachi waweze kununua huku akisema kuwa kwa sasa kuna wadudu hatari ambao wanashambulia mahindi jambo ambalo linazidi kuwakatisha tama wanachi wao.

Hata hivyo Madiwani hao kwa nyakati tofauti wamedai kuwa kuna wadudu ambao wameibuka na kuanza kushambulia zao la mahindi kwani ni chakula ambacho wanategemea hivyo wameimba idara ya kilimo kuendeleza tafiti ili kubaini wadudua hao kwa lengo la kuwatokomeza.
Powered by Blogger.