BASI LA WACHEZAJI DORTMUND LASHAMBULIWA KWA MILIPUKO, MECHI YASOGEZWA LEO JUMATANO
Basi la wachezaji wa Borussia Dortmund limeshambuliwa na imeelezwa kumekuwa na milipuko si mikubwa sana.
Milipuko hiyo imesababisha beki Marc Bartra kuumia na kupatiwa matibabu baada ya kuumizwa na vioo.
Hali
hiyo imesababisha mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Dortmund
dhidi ya Monaco, kusogezwa leo Jumatano badala ya Jumanne.
Mechi hiyo sasa itachezwa leo Jumatano lakini itakuwa mapema zaidi.