NAPE: REDIO ZIENDANE NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA HABARI


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na wadau Redio na vyombo vya habari kwa ujumla katika maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliyofanyika katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Jijini Dar es Salaam.
Picha na Habari na Raymond Mushumbusi
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amevishauri vyombo vya habari nchini hususani Redio kuendana na mabadiliko ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano inayokuwa kwa kasi.
Ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliofanyika katika Chuo Kikuu huria cha Tanzania na kusisitiza vyombo vya habari nchini hasa Redio kuendana na mabadiliko ya ukuaji wa Teknolojia ili kuenda sambamba na mabadiliko hayo.
Ameongeza kuwa Redio nchini zinatakiwa ziandae mikakati zaidi ya kuendana na mabadiliko hayo kwani ndio sasa dunia inapoelekea.
“Kutokana na mabadiliko ya Teknolojia mtu anaweza kurekodi tukio na kuliweka mtandaoni muda huo huku redio ikisubiri kuandika na kuhariri tukio hilo na kulirusha hewani tuliangalie hili kwa kina” Alisisitiza Mhe. Nnauye.
Amewasahuri waandishi wa habari nchini kuwa natabia za kusoma na kujua Taratibu na Sheria mbalimbali zinaendesha tasnia yao ili kuifanya tasnia kukua na kujengeka.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayub Riyoba amesema kuwa vyombo vya habari nchini hususani Redio vinatakiwa kuendana na mabadiliko ya teknolojia inayokua siku hadi siku ili kuleta tija katika utoaji habari kupitia Redio.
“Ndugu zangu wanahabari hasa wale kwenye Redio tuendane na mabadiliko ya teknolojia kwani Redio ni moja ya chombo cha mawasiliano kinachowafikia watu wengi kwa urahisi” Alisistiza Dkt Riyoba.
Powered by Blogger.