MWANDISHI WA HABARI KAMPUNI YA MWANANCHI COMMUNICATION ATOA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KWA BINTI SHULE YA SEKONDARI SIRARI.

MWANDISHI WA HABARI KAMPUNI YA MWANANCHI COMMUNICATION WAITARA MENG'ANYI  KULIA AKIKABIDHI BEGI KWA DIWANI WA KATA YA SIRARI NYANGOKO PAUL ILI AKAMKABIDHI BINTI AMBAYE MWANDISHI HUYO AMEJITOA KUSAIDIA VIFAA VYA SHULE AMBAPO AMETOA BEGI MOJA NA SHILINGI ELFU 30,000 KWA AJILI YA KUSHONA SARE ZA SHULE.
MWANDISHI AKITETA JAMBO NA DIWANI WA KATA YA SIRARI PAUL NYANGOKO.
DIWANI WA KATA YA SIRARI PAUL NYANGOKO AKIKABIDHI BEGI HILO KWA NIABA YA MWANDISHI WA HABARI LENGO NI KUSAIDIA BINTI HUYO AMBAYE AMENYIMA MAHITAJI YA SHULE BAADA YA KUKATAA KUKEKETWA.
BINTI HUYO AKIKABIDHIWA FEDHA SHILINGI ELFU 30,000 KWA AJILI YA MANUNUZI YA SARE YA SHULE  KWANI BINTI HUYO AMEDAI  KUWA TANGU APELEKWE KIDATO CHA KWANZA MPAKA SASA MAZAZI WAKE AMEKATAA KUNUNUA SARE HIZO.


Akikabidhi vifaa hivyo mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communication Waitara Meng’anyi amesema kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya kwenda kufanya mahojiano na binti huyo na kubaini kuwa wazazi wake wameshindwa kununua vifaa vya shule ili  kuendelea na masomo huku wakilazimisha binti huyo kukeketwa  na kuguswa na jambo hilo hivyo amejitolea kutoa msaada huo.

“Sisi waandishi wa habari siyo kwamba jukumu letu ni kuandika habari tu wakati mwingine tunapaswa kusaidia jamii  inayotuzunguka ili iweze kutimiza ndoto zake nimeamua kusaidia binti huyu baada ya kunisimulia kisa chake na kuguswa” alisema Waitara.

Aidha Mwandishi huyo ametoa msaada wa Begi Moja na shilingi Elfu3,000 kwa ajili ya kushona sare za Shule na kununua mahitaji mhimu ya shule.
Akikabidhi kwa niaba ya Mwandishi huyo Diwani wa kata ya Sirari Paul Nyangoko amezidi kuwaasa wazazi na walezi kuondokana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Binti Huyo ambaye hakutaka jina lake kutajwa mwanafunzi wa kitado cha pili shule ya sekondari Sirari amesema kuwa tangu apelekwe kidato ch kwanza mzazi maybe ni baba wake wa kambo hajawai kununua sare za shule mpaka sasa huku akishikilia madaftari mikononi.

Wazazi wangu hasa mama mazazi amekuwa akinilazimishwa kukeketwa sasa imekataa na nilivyoenda kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kijiji Baba, Mama na kaka walinipiga na kuniumiza sana huku kaka akinitishia maisha naomba serikali inisaidia alisema Binti huyo.
Powered by Blogger.