MVUA YA DAKIKA 10 YAZUA BALAA SHINYANGA USIKU HUU,NYUMBA ZAIDI YA 20 ZAEZULIWA NA UPEPO MKALI
Hapa ni katika shule ya MsingiViwandani iliyopo katika manispaa ya Shinyanga |
Nyumba zaidi ya 20 zimeezuliwa na upepo mkali wakati mvua ikinyesha usiku huu wa Januari 11,2017 katika manispaa ya Shinyanga.
Inaelezwa kuwa kuna taarifa ya vifo
ingawa mamlaka husika hajitoa taarifa kuhusu tukio hilo,tutawajuza pindi
tu tukipata taarifa za uhakika.
Vyanzo vya habari vya Malunde1 blog
vinasema mvua hiyo ya iliyoambatana na upepo pia imejeruhi watu kadhaa
katika kata ya Kitangiri manispaa ya Shinyanga.
Diwani wa viti maalum tarafa ya Ibadakuli katika manispaa ya Shinyanga
Zuhura Waziri (CCM) amefika katika baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa na
kujionea uharibifu uliojitokeza kufuatia mvua hiyo inayodaiwa kunyesha
kwa muda takribani dakika 10 tu majira ya saa tatu usiku wa Jumatano
Januari 11,2017.
Diwani huyo amesema mvua hiyo mbali na kuharibu nyumba zaidi ya 20 pia
madarasa manne na ofisi ya walimu katika shule ya msingi Viwandani
zimeezuliwa.
Amewaomba wasamaria wema kufika katika eneo hilo ili kutoa msaada kwa wananchi waliothirika na mvua hiyo.
Amewaomba wasamaria wema kufika katika eneo hilo ili kutoa msaada kwa wananchi waliothirika na mvua hiyo.
Jeshi la zimamoto limefanya jitihada za kuokoa mali mbalimbali
Taarifa kamili tutawaletea hivi punde