Mtoto amuua baba yake sababu ya asali






Jeshi la polisi linamtafuta mkazi wa kijiji cha Kitenga Walayani hapa mkoani Mara Bakari Bakari (32)  kwa tuhuma za kumpiga baba yake mzazi kichwani kwa kitu chenye ncha kali na kumsaabishia mauti.

Kamanda wa mkoa wa kipolisi Tarime /Rorya Andrew Satta amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kumtaa aliyeuawa kuwa ni Shaban Ramadhan (56) aliyefariki dunia baada ya kumkuta kiana wake akiiba asali yake kwenye stoo.

Satta alisema kuwa tukio hilo lilitokea katika kijiji cha kitenga januari 11 saa 4:00 usiku wakati marehemu Shaban ambaye ni mfanyabiashara wa asali alipofungua mlango wa stoo yake kwa lengo la kutunza mabaki ya asali.

Wakati akiingia ndani kijana wake aliyekuwa ameishaingia ndani ya chumba hicho kwa nia ya kutaka kuiba asali alimvamia baba yake na kumpiga kichwani kwa kitu chenye ncha kali na kumsababishia mauti hapo hapo.

Mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mji wa Tarime, Samwel Marindi alisema majira ya saa 4:00 usiku juzi alipigiwa simu na polisi wakimtaka afike katika eneo lake la kazi kupokea mwili wa marehemu ambao umehidhiwa kwenye chumba hicho.

Shuhuda wa tukio hilo Alex Chacha alisema walisikia yowe ikipigwa wakatoka nyumbani kuwenda kusaidia ndipo walimkuta mwili wa marehemu ukiwa kwenye chumba alichokuwa kikitumia kama stoo ya kuhifadhia asali na kupiga simu kituo cha polisi Sirari.

“Polisi walikuja wakafanya uchunguzi na wakauchukuwa mwili kuupeleka Bomani ulipotunzwa, chanzo kijana alikuwa nataka kuiba asali ya baba yake,” alisema Chacha.

Chacha ambaye ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Buriba Kata ya Sirari alisema kuwa marehemu nakusanya asali na kuisambaza kwa wanunuzi wilayani Tarime na nje ya Tarime.

“Hatujajua kwa nini aliamua kumsahambulia baba yake hadi kumsababishia mauti, kwangu hii ni familia marafiki umekuwa msiba mkubwa,” alisema Chacha.

Hili ni tukio la aina yake kutokea katika mji wa Sirari baada ya lile la desemba 29 mwaka  Tajiri Robert Mwikwabe alipompiga Risasi kwenye  paji la uso Maite Amilly (17) mwanafunzi wa kidato cha tatu katika sekondari ya Sirari na kufariki dunia hapo hapo wakati wakigombea pumba za Mchele.
Mwisho.


Powered by Blogger.