Kwa upande wake Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche alisema
kuwa nia ya Viongozi ambao ni wawakilishi wa wanachi ni kuwaletea wananchi
maendeleo ya haraka na kutoa vipaumbele vyenye tija ikiwwemo Miundombinu ya
barabara, Elimu Afya na Maji,
“Ukiangalia katika bajeti hii wameleta kukarabati Canteen
kwa kiasi cha shili Millioni 60 tumekataa na kuzielekeza katika miundombinu ya
barabara kwa sababu tumetumwa na wanachi hatuna budi kupendekeza miradi yenye
vipaumbele vya kuwanufaisha wananchi wote” alisema Heche.