DC LUOGA AKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA KAYA 100 KUTOKA KWA DIWANI KOMOTE KATA YA NKENDE CCM.

MKUU WA WILAYA YA TARIME GLORIOUS LUOGA AKIONESHA WANACHI MOJA YA KADI YA BIMA YA AFYA ZILIZOTOLEWA KWA KAYA 100 NA DIWANI WA KATA YA NKENDE CCM DANIEL KOMOTE IKIWA NI MOJA YA KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA CHAKE.
MKUU WA WILAYA YA TARIME AKISAINI KATIKA KITABU CHA WAGENI.
DIWANI WA KATA YA NKENDE CCM DANIEL KOMOTE AKIELEZA KWA MKUU WA WILAYA YA TARIME LUOGA JINSI UJUENZI WA MADARASA SHULE YA MSINGI MAGENA UNAVYOENDELEA.
DIWANI WA KATA  YA NKENDE CCM AKIELEZA UMHIMU WA KUJIUNGA NA MFUKO WA JAMII (CHF) BAADA YA KUKABIDHI KADI ZA CHF  KWA KAYA 100

MTENDAJI WA KATA YA NKENDE MARWA KONDOKO AKISOMA TAARIFA YA KATA HIYO.
AMINA IBRAHIMU MENEJA WA BIMA ZANZIBA AKIELEZA UMHIMU WA KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA YA JAMII.
DIWANI WA VITI MAALUMU CCM SALMA ABUBAKHAR AKIONGEA NA WANACHI WA KATA YA NKENDE .
MGANGA MKUU HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME CALVIN MWASHA AKIONGEA NA WANANCHI NA KUSISITIZA SUALA ZIMA LA KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA UKIWEMO MFUKO WA (CHF)
KATIBU TAWALA WILAYA YA TARIME JOHN MARWA AKIONGEA NA WANACHI WA KATA YA NKENDE.
MKUUWA WILAYA YA TARIME LUOGA AKIKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA (CHF) KWA WANUFAIKA WAKIWEMO WAZEE, WALEMAVU NA WATU WASIJIWEZA ILI WAWEZE KUTIBIWA VYEMA.
MWENYEKITI WA MTAA WA SONGAMBELE CHADEMA PAMBA CHACHA  AKIKABIDHIWA KADI KUMI KWA AJILI YA WANACHI WAKE BAADA YA DIWANI WA KATA YA NKKENDEDANIEL  KOMOTE (CCM) KUJITOLEA KULIPIA KAYA HIZO MBALI NA KULIPIA KAYA 100 KATIKA KATA YAKE "ALISEMA KUWA AKIPITA KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIKUWA UNAFANYIKA MTAA SONGAMBELE  KATA YA SABASABA ALIKUTA AGENDA YA KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA NA KUWIWA NDIPO  ALIAMUA KUKATIA FAMILIA KUMI
MMOJA WA WANACHI AKIONESHA KADI YA BIMA YA AFYA ALIYOPEWA


Diwani wa Kata ya Nkende Daniel Komote(CCM) ameziwezesha kaya 100 kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) ambapo watu 600 kutoka kaya hizo wamenufaika wakiwemo Wazee na Walemavu.



Diwani huyo alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa lengo la kutimiza ahadi ikiwa ni pamoja na kutekeleza ilani ya chama chake.



“Nimetoa Bima hizi kwa kaya 105 mpaka sasa lakini hata wakifikia 115 nitawalipia ili waweze kupata huduma ya Afya kwa uhakika mwaka mzima” alisema Komote.



Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga amekabidhi kadi za CHF kwa  familia hizo zilizonufakika na msada huku na akiwataka wanachi wengine kuiga mfano huo na kuweza kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii



Naye Mganga Mkuu Halmashauri ya Mji wa Tarime Calvin Mwasha naye amezidi kuwasissitiza wanachi  kujiunga na mifuko ya bima ya Afya huku akisema kuwa suala la upumgufu wa madawa kwa sasa halitakuwepo kwani serikali imejipanga vyema katika kuboresha huduma ya Afya.

Nao baadhi ya Wananchi ambao ni wanufaika wameshukuru jitihada za diwani huyo  kwa kuwawezesha kujiunga na mifuko ya Bima ya Afya huku wakisii viongozi wengine kuiga mfano huo.
PICHA ZOTE NA CLEO NEWSTZ  KWA HABARI PIGA SIMU NO 0766424928
Powered by Blogger.