Kutokana
na kutokea kwa matukio mbalimbali hapa nchini yaliyoibua sintofahamu kwa
wananchi pamoja na serikali nakuwaacha
vinywa wazi kwa kuwasababishia hasara kubwa ikiwemo tetemeko la ardhi kutokea
hivi karibuni mkoani kagera na
kusababisha maafa, makubwa katika kitongoji cha nyabikondo kijiji cha kewanja Nyamongo Wilayani Tarime mkoani
Mara wakazi wa eneo hilo wamejikuta wakikosa makazi na kulala nje takribani siku tatu pamoja na mali zao baada
ya nyumba zao za nyasi kumi na moja kuungua moto zenyewe kwa nyakati
tofauti na chanzo cha matukio hayo kutojulikana kwani wananchi wamekuwa wakiona
nyumba hizo zinawaka moto ghafla kwani tukio hilo limeanza Septemba saba mpka septemba kumi huku baadhi wakidai kuwa ni ushirikina .
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti wananchi hao wakiwemo wahanga wa matukio hayo
wamesikitishwa na hali hiyo huku wakibaki na sintofahamu ikiwa ni baada ya mkuu
wa wilaya ya Tarime Gloriuos Luoga kufika maeneo hayo na kuzungumza na wananchi
, viongozi wa serikali ,wazee wa milapamoja na viongozi wa dini wakiwemo na kusema kuwa serikali inaendelea na
uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo huku akiwasii kuwa waondokane na
imani za kishirikina.
Akithibitisha
kutokea kwa matukio hayo ya kuchomwa kwa nyumba hizo kumi na moja Mtanzania
Omtima ambae ni mwenyekiti wa kijiji cha kewanja amesema kuwa baada ya kutokea matukio hayo
wamewza kufanya taratibu zote lakini mpaka sasa hata wao hawajabaini chanzo cha
tukio hilo na kudai mpaka sasa hivi wananchi wake hawana makazi.
Hata
hivyo wazee wa milia wamedai kuwa watakaa kwa ajili ya kuangalia suala hilo kwa
kina huku wakiomba serikali kuendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.
Hali
hiyo imempelekea mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luoga ambae ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na
usalama kufika maeneoambayo yamekumbwa na janga hilo na kushuhudia nyumba hizo zilizo unguzwa kwa
moto ambapo amewataka wananchi kuchukua tahadhari mapema kutokana na matukio
hayo .
Hata
hivyo serikali wilayani Tarime kupitia
halmashauri ya wilaya hiyo imeweza kutoa msaada kwa wahanga kiasi cha shilingi
milioni mbili na laki mbili kwa kupatiwa wahanga kumi na moja wa nyumba hizo
kiasi cha shilingi laki mbili huku mkuu wa wilaya akiongoza zoezi la kuchangia
wahanga hao nakupatikana shilingi laki
tatu kwa ajili ya kupatiwa mahitaji kama chakula .
|