Matiko achukua fomu ya kuwania jimbo la Tarime.

Picha ya mbu nge wa viti maalumu kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Mara Esther Matiko akionesha fomu yake mbele ya waandishi wa habari katika ofisi ya Chama Wilayani Tarime Mkoani Mara


Matiko achukua fomu ya kuwania jimbo la Tarime.


Mbunge wa Viti maalumu kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa  wa Mara Esther Matiko amechuku fomu ya kuwania jimbo la Wilaya ya Tarime kupitia Chadema kwa lengo la kuweza kuwatumiakia watanzania ili kuleta Maendeleo.

Mbunge huyo aliwasili jana katika Ofisi ya Chadema Wilaya kwa ajili ya kuchukua  fomu hiyo na baadakueleakea katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shamba la bibi nakuweza kuongea na watanzania juu ya mustakabali wa Nchi huku akiwataka kuwa waewze kufanya maamuzi sahihiya kuchagua kiongozi bora kulingana na matendo yake mazuri.

Mbunge huyo alisema kuwa Kutokana na mapokezi aliyoyapokea tayari yameonesha jinsi gani wako na kiu kiasi gani hivyo endapo chama kitaweza kumpitisha ataweza kufanya kazi ipasavyo kwa lengo la kubadili maisha ya Wananchi ususani Wilayani Tarime.

“Leo nimepokelewa vizuri sana nimeamini kuwa mfume dume ambao umeenesha unaenda kudhiilishwa kuwa sasa haupo kinachoitajika ni kiongozi wakuweza kuwatetea wananchi na kuwasemea ili waweze kupata maendeleo” alisema Esther.

Matiko atarudisha leo  fomu katika ofisi za chama cha Demokrasia na maendeleo chadema Wilaya  baada ya kuijaza na badae ataweza kuongea na Watanzania.

Kwa Upande wake  katibu wa Vijana wilaya ya Iringa Mjini Reya Mleleu alisema kuwa hiki ni kipindi cha wanawake kuonesha uwezo wao kwani wamekuwa wakidanaganyika kwa muda mrefu na sasa wameamua kusaka maendeleo.

Moses Matiko Visiwa ambaye ni Mwenyekiti wa Barala za vijana Chadema Wilaya ambaye pia ni Mwanasheria wa Chama hicho Kanda ya Serengeti ambaye pia naye ni kati ya watanagazania14 ambao tayari wametangaza kuwania jimbo la Tarime alisema kuwa kikubwa kilichomusukuma kuwania nafasi hiyo ni kutumia fursa takayo pewa katika kusimamia rasimali za watanzania ambazo ikiwa ni pamoja na ukwepaji wa kodi za makampuni ya kigeni ambayo yamewekeza katika nchi ya Tanzania.
                                 …….Mwisho…..
Powered by Blogger.