TTC TARIME WAHOFIA JKT WATAKA IONDOLEWE,WAZIRI KAWAMBWA ASEMA HAIWEZEKANI.

Picha ya waziri wa Elimu Nchini Shukuru Kawambwa akiongea na wanachuo wa Chuo cha Ualimu TTC Tarime Mkoani Mara  katika ukumbi wa chuo hicho.

SERIKALI imesema kuwa  haitasitisha mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa walimu  kwakuwa mafunzo hayo yanawajengea walimu ukakamavu, nidhamu na kujua shughuli mbalimbali za uzalishaji zikiwamo za kilimo.
Akijibu swali la Jovenal Thomas Airo mmoja kati ya wanafunzi wa chuo cha ualimu Tarime  ndani ya ukumbi wa chuoni jana lililohoji  kuna manufaa gani mwalimu kwenda JKT ? kwa madai kuwa mpango huo hauna manufaa zaidi ya walimu kufariki wakiwa JKT kutokana na matatizo ya kiafya,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Shukuru Kawambwa alisema kuwa Mpango huo ni mzuri  kwa madai kuwa hata mika ya nyuma walimu walikwenda JKT baada ya kuhitimu mafunzo ya chuo cha ualimu.
Kawambwa alisema kuwa   mafunzo ni miezi 3 tofauti na miaka ya nyuma ambayo yalitolewa kwa muda wa mwaka mmoja hivyo anashangaa kuona  baadhi ya wanafunzi wakiogoma na kuhofia mazoezi ya JKT.
“Msiogope KJT nyie miezi mitatu tu mnaogopa! Sisi tulifanya mwaka mmoja tena mimi nilienda JKT Bulombola Kigoma ambako ndiko kunaogopwa sana kwa mazoezi makali lakini sikuogopa  istoshe mazoezi nikuwafanya kuwa wakakamavu na nidhamu pia”alisema Kawambwa.
Waziri huyo  alisema kuwa zoezi hiilo ni jambo zuri  kuwepo nakwamba ilikuwa ni makosa kusitishwa miaka ya nyuma kutokana na ukosefu wa fedha za uendeshaji  nakwamba kwa sasa Serikali  ililitazama hilo na kuona numuhimu kurejesha mazoezi hayo.
Wakati huohuo,Waziri huyo  amesema kuwa Serikali itajitahidi kuhakikisha ina tatua changamoto zinazoikabili chuo cha ualimu Tarime yakiwamo madeni ya wakufunzi, na ukarabati wa majengo ya chuo.
Kawambwa alisema kuwa  Serikali imejitahidi kupunguza madeni ya walimu ambapo pia  inatarajia kujenga vyuo vya ualimu vyenye hadhi ya kisasa tofauti na vyuo vilivyopo sasa ambavyo vimeonekana majengo yake yamepitwa na wakati
“Tunajitahidi kutatua changamoto kwa baadhi ya vyuo  hivyo nahaidi Tarime nayo kwa baadae yatajengwa majengo ya kisasa tumeona tuanze  ujenzi kwa vyuo ambavyo vinachangamoto kubwa zaidi ya Tarime lakini pia tumejitahidi kupunguza madeni ya walimu yatalipwa ila nawatahadhalisha walimu ambao wameandika madeni ya uongo’Alisema kawambwa.
Mkuu wa chuo cha ualimu Tarime Samwel Magige alisema kuwa chuo  hicho kinakabiliwa na mapungufu kadhaa yakiwamo ya  ukosefu wa watumishi,wakufunzi,Nyumba za watumishi,uchakavu wa miundombinu,Madeni ya wazabuni hususani chakula,fedha za rikizo kwa watumishi na kusababisha wasiende rikizo.
Magige alisema kuwa mbali na changamoto hizo Chuo kinaendelea na ukarabati wa baadhi ya majengo ambapo  sasa wanaendelea na ujenzi wa Mabweni ujenzi uliogharimu milioni 14 na unaendelea nakwamba chuo kina idadi ya wanafunzi 655 na wakufunzi 40.
Powered by Blogger.