Makatibu wilaya CHADEMA Mkoa wa Mara wapewa pikipik

Pikipiki zikiwa katika ofisi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Musoma mjini ili kuweza kuwagawia makatibu wilaya wa chama hicho.



CHAMA cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Mara kimekabidhi pikipiki 8 kwa makatibu wa wilaya   mkoani hapa zenye thamani ya Millioni 16 ili kurahisisha utendaji kazi wa chama hicho katika wilaya zao.
Makatibu  waliokabidhiwa leo  pikipiki hizo ofisi ya wilaya ya Musoma mjini ni kutoka wilaya za Serengeti,Rorya,Musoma mjini, Musoma Vijijini,Bunda,Butiama,Tarime na jimbo la Mwibara.
Katika kukabidhi pikipiki hizo katibu wa chama cha demokrasia na Maendeleao (CHADEMA) Ctihacha Heche, aliwataka makatibu hao wazitumie pikipiki hizo walizopewa kwa makatibu hao wazitumie kwa ajili ya shughuli za chama.
“Pikipiki hizi naomba tafadhari zifanye kazi za chama zisiende kusumbua vijana wetu wa bodaboda na kutumika vibaya kwa mambo ya starehe tukibaini hilo kwa ushahidi vya kjutosha tutachukua hatua”alisema katibu wa chadema mkoa mara,Heche.
Katibu alizidi kusisitiza kuwa watendaji hao wasitumie vibaya vyombo hivyo vya moto kwa ajili ya maslahi yao binafsi suala ambalo linaweza kuleta migogoro ya hapo badae
Naye Mhazina wa kanda mashariki Haire Tarai katika kuzindua rasmi pikipiki hizo alisema kuwa  kanda ya ziwa mashariki ina majimbo21 na majimbo hayo yameweza kupata pikipiki hizo ambazo zimeghalimu shilingi milioni 42.
“Makao makuu wametoa pikipiki hizi na zimeghalimu fedha kubwa nchi nzima pikipiki zimeghalimu zaidi ya billion 2.7 kwa zaidi ya wilaya na majimbo 130 ‘’ alisema Haire.
Kwa upande wa makatibu hao kwa niaba yao Johness Sando wa Musoma Vijijini, alisema kuwa, piki piki hizo zimewawezesha kuwarahisishia usafiri katika shughuli za chama.
Aidha piki piki hizo ni moja ya utekelezaji wa mipango ya kuimalisha chama kiweze kushiriki vyema katika chaguzi za serikali za mitaa na mkuu wa  mwaka huu na mwakani.
Piki hizo ilielezwa kuwa ni sambamba na magari yanayotarajiwa kugawiwa kila makatibu wa mkoa yatakayo tumiwa katika shughuli za chama hicho kabla ya uchaguzi wa mwaka kesho.
Hafla hiyo baada ya kumalizika kuliendeshwa kikao cha ndani na makatibu hao waliopanga mipango na maelekezo ya chama na  katibu wa mkoa huo .
 -----------------------------------mwisho-------------------------------------------------         
Powered by Blogger.