SIKILIZA AUDIO; WANAFAMILIA WATATU WAFA KWA KULA ASALI TARIME
Watu watatu wa familia moja wakazi wa kijiji cha
Nyantira kata ya Nyansicha Wilayani hapa mkoani Mara wanadaiwa kufariki
dunia kwa kula asali.
Kaimu
kamanda wa mkoa wa polisi Tarime/Rorya Sweetbert Njewike akiongea kwa
njia ya simu akiwa Shirati wilayani Rorya amesema hana taarifa hiyo
ofisini kwake.
Mwenyekiti
wa kijiji cha Nyantira James Chacha amesema tukio hilo kutokea juni 7,
8 na 9 na kuzua taharuki kijijini hapo kutokana na aina ya vifo vya
wanafamilia hao watatu kufariki kwa kufuatana.
Amewataja
waliofariki kuwa ni Kerato Nyangera( 70) Regina Kerato (50) na Samwel
Kerato (12) mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Nyantira.
Chacha
amesema "juni saba tulizika mzee mzee, baada ya kumkimbiza kituo cha
afya Muriba,baada ya saa 12 akafariki,tukamleta nyumbani
kuzika,tulipomaliza maziko mtoto naye akawa kwenye hali mbaya,
tukamkimbiza kituoni, akafa, siku tunazika akaanza mama naye akafa
pia,"alisema.
Ameongeza kuwa kufariki kwa watu hao kwa mfuatano kijiji kimeingizwa na wasiwasi kwa kuwa wazazi hao wameacha watoto wadogo.
"Wameacha watoto wanne mmoja alikuwa anamuona bado,"alisema Chacha.
Mganga
mfawidhi wa hospitali ya Tarime Mkumbo Odari alisema "asali kama asali
haina madhara kwenye mwili wa binadamu isipokuwa pale inakuwa
imechanganyikina na sumu ndipo inapoweza kuleta madhara, na hii ndiyo
maana inatumiwa kama dawa, kwenye chakula kupaka kwenye mikate,"
alibainisha Odari.
Sunday
Magacha ni diwani wa kata ya Nyansicha alisema hadi sasa chanzo cha
vifo vya wanafamilia hao hakijajulikana na uchunguzi bado unaendelea ili
kufahamu nini chanzo licha ya kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na
kituo cha afya Muriba ulionyesha kuwa walikuwa wamekula sumu.
Alisema tukio hilo lilikuwa la kwanza na la aina yake ambalo limeacha wananchi wameathirika kisaikolojia
"Tunaomba
Serikali kuwa nyepesi inapopewa taarifa isifanyike kazi haraka na
wananchi wajifunze kutokana na matukio hayo na kuwa makini ili kuepuka
madhara kama haya,"alisema Magacha.
Wakazi
wa kijiji cha Nyansicha walisema kuwa vifo hivyo vilikuwa vya
kushitukiza kwani kwa siku tatu kuzika watu wa familia moja kimezua
maswali mengi kwenye vichwa vyao huku watoto wadogo wakiachwa bila
malezi yao.
"Watu zaidi
ya watano walikuwa asali na huyu mee akilima kwa ndugu yake akala kisha
akapeleka nyumbani kwake lakini tulishangaa kusikia kuwa yeye na mkewe
na mtoto wamefariki tena kwa kufuatana, alisema jirani familia hiyo
Magabe Iroga.
SIKILIZA AUDIO KUHUSU TUKIO HILO